Muhimu: Kwa maelezo muhimu kuhusu matumizi salama ya kifaa na betri yako, soma maelezo
ya ”Kwa usalama wako” na ”Usalama wa Bidhaa” katika mwongozo uliochapishwa wa mtumiaji,
au kwenye www.nokia.com/support kabla utumie kifaa. Ili kujua jinsi ya kuanza kutumia kifaa
chako kipya, soma mwongozo uliochapishwa wa mtumiaji.
Usiunganishe kwenye bidhaa ambazo zinaunda wimbi la kutoa, kwa kuwa hii inaweza kuharibu
kifaa. Usiunganishe chanzo chochote cha stima kwenye kiunganisha cha sauti. Ukiunganisha
kifaa chochote cha nje au kifaa chochote cha kichwa kando na zile zilizoidhinishwa kutumiwa
na kifaa hiki, Kiunganishi cha sauti, kuwa makini sana na viwango vya sauti. Sehemu nyingine
za kifaa hiki zina sumaku. Vitu vya chuma vinaweza kuvutwa na kifaa. Usiweke kadi za karadha
au vitu vingine vyenye kutumia hifadhi ya sumaku karibu na kifaa hiki, kwa sababu maelezo
yaliyohifadhiwa kwenye vitu hivyo yanaweza kufutika.
Baadhi ya vifaa vya ziada vilivyotajwa katika mwongozo huu wa mtumiaji, kama vile chaja,
vipokea sauti vya kichwani, au waya wa data, vinaweza kuuzwa kando.
Dokezo: Unaweza kuweka mpangilio ili simu yako iombe msimbo wa usalama ili kulinda
faragha na data yako binafsi. Chagua Menyu > Mipangilio > Usalama > Kilinzi cha vitufe >
Msimbo wa usalama kisha uweke msimbo. Hata hivyo kumbuka kwamba unahitaji kukumbuka
msimbo huo, kwani HMD Global haiwezi kuufungua au kuuruka.
SANIDI NA UWASHE SIMU YAKO
Nano-SIM
Muhimu: Kifaa hiki kimeundwa ili kutumiwa na SIM kadi ya nano pekee (angalia mfano).
Matumizi ya kadi zisizotangamana za SIM zinaweza kuharibu kadi au kifaa, na zinaweza
kuharibu data iliyohifadhiwa kwenye kadi.
Kumbuka: Zima kifaa na usiiunganishe na chaja au kifaa kingine chochote kabla ya kubandua
vifuniko vyovyote. Epuka kugusa visehemu vya elektroniki wakati wa kubadilisha vifuniko
vyovyote. Daima hifadhi na kutumia kifaa kikiwa na vifuniko vyake vimewekwa.
Ikiwa una simu ya matundu mawili ya SIM, ingiza kadi yako ya SIM kwenye tundu la SIM1 na SIM
ya pili kwenye tundu la SIM2. Kadi zote mbili za SIM zinapatikana kwa wakati mmoja wakati kifaa
hakitumiki, lakini kadi moja ya SIM inapokuwa ikitumika, kwa mfano, wakati wa kupiga simu, ile
ya pili haipatikani.
Kidokezo: Ili kujua ikiwa simu yako inaweza kutumia SIM kadi 2, angalia lebo kwenye sanduku
la mauzo. Ikiwa kuna misimbo 2 ya IMEI kwenye lebo, una simu yenye SIM mbili.
Ingiza kadi ya kumbukumbu
1. Telezesha chini kishikizi cha kadi ya
kumbukumbu kisha ukifungue.
2. Weka kadi ya kumbukumbu kwenye tundu.
3. Funga kishikizi na ukitelezeshe juu ili
kukifunga.
Kidokezo: Tumia kadi ya kumbukumbu ya microSD yenye kasi, na ya hadi GB 32 kutoka kwa
mtengenezaji anayefahamika.
Washa simu yako
Bonyeza na ushikilie .
CHAJI SIMU YAKO
Betri yako imechajiwa nusu kiwandani, lakini utahitajika kuichaji upya kabla uweze kutumia simu
yako.
Chaji betri
1. Chomeka chaja kwenye soketi ya ukuta.
2. Unganisha chaja kwenye simu. Ukimaliza, chomoa chaja kwenye simu, kisha kwenye soketi
ya ukuta.
Kama betri imeisha moto kabisa, huenda ikachukua dakika kadhaa kabla ya kiashiria chaji
kuonyeshwa.
Kidokezo: Unaweza kuchaji kwa kutumia USB wakati umeme wa ukutani haupatikani. Ubora
wa nishati ya kuchaji kwa USB hutofautiana, na huenda ikachukua muda mrefu kuchaji kuanza
na kifaa kuanza kufanya kazi.
VITUFE
Tumia vitufe vya simu
• Ili kuona programu na vipengele vya simu yako, kwenye skrini ya mwanzo, chagua Menyu .
• Ili kwenda kwenye programu au kipengele, bonyeza kitufe cha kutambaza juu, chini,
kushoto, au kulia. Ili kufungua programu au kipengele, bonyeza kitufe cha kutambaza.
• Kurudi kwa skrini ya mwanzo, bonyeza kitufe cha kukata simu.
• Ili kubadilisha sauti ya simu yako wakati unaongea kwenye simu au unaposikiliza redio,
bonyeza vitufe vya sauti.
Funga kicharazio
Ili kufunga vitufe, funga tundu. Ili kufungua vitufe, bonyeza kitufe cha kutelezesha kisha
uchague Fungua > * .